Taarifa na Tangazo kwa wana IFM, CBE, DIT, DMI, MA, na TPCS

TAARIFA KUTOKA OCM

OCM imefanikiwa kumaliza vikao vyake na ofisi za serikali za mitaa kwa kata ya kigamboni na kata ya Tungi. Ikijumuisha wabunge au wawakilishi wa maeneo na wamiliki wa Hostel na vyumba kwa kila ofisi ya serikali ya mtaa.

Ofisi za serikali za mitaa ambazo OCM imefanikiwa kufanya vikao navyo pamoja na wamiliki wa Hostel na  Vyumba ni Ferry, Kigamboni, Tuamoyo, Tungi, Magogoni na Muungano.

Hivyo basi, maazimio ya vikao hivyo ilikuwa kupata utatuzi madhubuti wa suala la ulinzi na usalama kwa wanafunzi wenzetu na mazingira wanayoishi kiujumla.

Kwa wamiliki wa Hostel wote kwa pamoja katika kata ya Kigamboni na Kata ya Tungi, wanatakiwa kuweka walinzi private katika Hostel zote zikaliwazo na wanachuo.

Na kwa wanaoishi katika maeneo mbalimbali katika kata hizo mbili, vilevile suala la ulinzi na usalama tutalisimamia kwa kushirikiana na afisa mtendaji kata ya Kigamboni na Afisa mtendanji kata ya Tungi. Pamoja na OCD kata ya Tungi. Pia tukishirikiana na ofisi za serikali za mitaa kutoa walinzi shirikishi kwa kila eneo.

TANGAZO KUTOKA OCM

OCM inapenda kuwatangazia wanachuo wote wa IFM, CBE, DIT, DMI, MA, & TPCS kuwa tunawaomba wanachuo wetu wasikae sehemu ambazo OCM haitaweza kuwafikia, bali tunapendekeza wanachuo wakae sehemu ambazo tunazitambua na ni rahisi kuwafikia.
Sehemu hizo ni:

KATA YA KIGAMBOMBONI:
i)                    Ferry
ii)                   Kigamboni
iii)                 Tuamoyo

KATA YA TUNGI
i)                    Tungi
ii)                   Muungano
iii)                 Magogoni

Na kwa wale wasiotaka kuishi Kigamboni, tutawatafutia makazi katika sehemu zifuatazo:
i)                    Kariakoo
ii)                   Magomeni

iii)                 Kinondoni

KWA MAELEZO ZAIDI FIKA OFISI YA SERIKALI YA WANAFUNZI YA CHUO CHAKO
Share on Google Plus

About UPStream Telecom

0 comments:

Post a Comment