Onyo kwa matumizi ya lugha chafu katika mitandao dhidi ya serikali ya wanafunzi IFM-SO


TANGAZO

Ni haki ya kila  mwanafunzi kutoa maoni, kushauri au kuikosoa serikali ya wanafunzi ifm ili kujenga chuo cha ifm. Lakini  mwanafunzi  ataruhusiwa  kufanya hivi vitu vitatu kwa nidhamu, busara na hekima. Hivyo basi kwa yeyote yule atakayeonesha utovu wa nidhamu kama vile kutumia lugha chafu katika mitandao ya kijamii kama whatsapp dhidi ya  serikali ya wanafunzi ifm-so hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Kwa sababu hiyo serikali ya wanafunzi (IFM-SO) ingependa  kuwataarifu viongozi wote wa makundi ya whatsapp( group admins) kuwa  makini na wajumbe(members) wao katika makundi yao hayo.Ikitokea mjumbe(member) yeyote kafanya utovu wa nidhamu basi group admin atatakiwa kumuwajibisha mjumbe huyo kisheria. Kinyume na hivyo mkuu wa kundi atawajibishwa na serikali ya wanafunzi IFM-SO kamati ya nidhamu.
Share on Google Plus

About UPStream Telecom

0 comments:

Post a Comment