IFM-SO ikishirikiana na Uhai Tanzania kutoa nafasi za ufadhili maalumu wa elimu kwa wasichana maombi hadi 31 jan 2017

Tangazo

Ufadhili Maalum Elimu kwa Wasichana Tu: 2016-2025

Chini ya Ufadhili wa Marafiki Bora wa Mama na Elimu Kwa Mtoto wa Kike [The Good Friends of Mothers and Girls Education]. Uhai Tanzania ni shirika la Afya ya Umma, lililoanzishwa lililosajiliwa 01.07.2011 kwa Na.84286 chini ya sheria za Mashirika ya Brela. Kwa sasa linafanya kazi ya Kuzuia vifo vya Uzazi kwa Wanawake Wajawazito, kwa kupitia kutoa elimu ya masomo ya darasani [fomrla education] Kwa wasichana tu.

Shirika linapenda kuwatangazia makundi haya [1] Wasichana ndani ya jamii [Umma] na [2] wanawake na wanaume wanafunzi wa kawaida-madarasa ya Kiingereza, Elimu ya masomo ya Sayansi, Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma, Eosiolojia [Sociology], na [3] wanawake na wanaume viongozi wanaotaka kufadhiliwa kuomba Ufadhi Maalum Kwa masomo ya Mwaka wa Masomo 2017 tu. Pia Shirika linawahimiza wazazi nchini Tanzania, Afrika na Duniani kuwawezesha  Wasichana, watoto wao wa Kike wanaotaka kufadhiliwa Masomo kuomba. Tangazo hili ni kwa nafasi za Umma kwa ujumbla na sio chuo au jamii fulani.

Wanafunzi chini ya Programu hii ya Ufadhili watasoma katika shule zifuatazo: Makongo, Jangwani, Zanaki, Morogoro, Dar es Salaam Baptist, Ubungo Modern, Loyola, na Educare. Shule za Msinigi ni Grace [Sinza], Atlas [ Ubungo], Sunrize [Mikocheni], Vyuo vikuu ni Chuo Kikuu cha Dar es salaam, SUA, Chuo Kikuu cha Tiba Shirikishi [Muhimbili], Chuo Kikuuu cha Ardhi, na nyuo vikuu vya nje ya Tanzania-ndani ya Africa na Ulaya.
Masomo ya:

Ngazi za masomo ni Chekechea, Msingi na /Kozi Maalum ya Kiingereza, Kurudia Mitihani, QT, na masomo ya O level, A level, na masomo ya QT, Vyuo vya Ufundi, Utalii, Ujasiriamali, na Vyuo Vikuu.

Huduma za Ufadhili: Ufadhili utatoa Ada ya masomo [Karo], Usafiri wa kwenda na kurudi nyumbani wakati wa likizo, vifaa vya darasani, vitabu vya mwanafunzi mwenyewe, kula, Bweni, malazi, matunzo ya muhimu kwa msichana.

Masharti ya Jinsi ya kuandika na kutuma barua ya Maombi
Wasichana na wanawake, na wanaume waandike barua ya Mkono ya Kiswahili [isichapishwe] aitume kwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji Uhai Tanzania, S.L.P 70913,Dar es Salaam, na au kukusanya katika semina na shughuli zetu Kila jumapili Ubungo Dar es salaam [piga simu kujua]: Wazazi wa watoto wa Chekechea waandikie barua watoto wao.
Ada ya Maombi isiyorudishwa:
·         Maombi ya Chekechea: Tsh 15,000=;     Maombi ya Msingi na O level: Tsh 15,000/=;
·         Maombi ya Kidato cha 5, Vyuo vya Ufundi, Utalii, Ujasiriamali, na Vyuo Vikuu: Tsh 20,000/=.
Mwisho wa maombi :   14 April 2017
Viambatanisho
Barua iambatane na
·         Picha za rangi 5 passport size;
·         Vivuli/nakala za Maotokeo  kila ngazi ya masomo kwa aina ya maombi ya taaluma.
·         Ada ya Maombi au lisiti HALISI [original] iliyolipia pesa Benk CRDB, Benki Akaunti 0152392952700, Jina la Akaunti Uhai Tanzania, iliyotajwa juu. au PESA TASLIMU iletwe katika semina wakati wa kuomba  tu pamoja na barua ya maombi {HAKUNA FOMU ZA MAOMBI} na hakuna ada ya kusajili, na hakuna mtihani
MUHIMU: Kwanza
Watakao someshwa chini ya Ufadhili huu, mbelini ndani ya mika 10 na mingine 20  [yaani miaka 30 ya programu hii] ijayo wengine watasoma Bure na wengine  kwa punguzo kubwa sana na kwa manufaa zaidi.
MUHIMU: Pili
Waombaji walio Dar es salaam wanatakiwa kuhudhuria Shughuli za Uzinduzi wa kitaifa na Kimataifa 4 March 2017.
Waombaji waliochaguliwa kuanza kusoma kutoka Mikoani wataarifiwa kupitia vymbo vya habari na mawasiliano yaliyotumika kuomba.
Pili huma za usafiri zitakuwa kwa mabasi ya Daraja la Kati na daraja la Kwanza tu ya Makampuni ya Arusha One, Dar Express [Arusha to Dar] , Dar Lux  Tunduma, Mbeya , Kahama na Mwana –Arusha Nairobi to Dar] , Shabiby [Dodoma to Dar], NBS [Kigoma, Tabora to Dar], Tashirif, Mining Nice, Superfeo [Songea, Iringa, Njombe, Morogoro to Dar], Falcon [Tarime, na Mtukula- Bukoba Mwanza, Lusaka, Harare,to Dar]. Ota High Class, Trinity,  [Kigali-Kagera-Dara],
Wazazi/waombaji wanaruhusiwa kupiga Simu 0714 41 81 90 kuulizia taratibu za jinsi ya kutuma maombi ili wasikwame.  [Wanafunzi wa SUA waliohudhuria Semina zetu June 2015 wanahimizwa Kuomba].
Sehemu ya pili ya Ufadhili ni Malipo ya Ada Maalum. Wazazi wanaotaka kulipia sehemu ya Ada bila kuchujwa, Ada zipo wawasiline nasi.
Wasicha wanaofanya kazi za ndani [housegirls], waliokatisha masomo, walipata mimba na kuacha shule, wanaoshindwa kulipa karo, waliofeli mitihani, waliokosa ufadhili, wanaosoma QT, wanaotoka familia bora , n.k wanaruhusiwa kuomba ndani na nje ya Tanzania wanaruhusiwa kuomba. Wazazi wanaotaka kulipa ada moja kwa moja waandike barua na waiambatanishe katika barua ya Mwanafunzi kuwa wapewe nafasi za kulipa sehemu ya Ada Maalum yenye Punguzo a Ofa Kubwa].
Imetolewa na
Mkurugenzi Mtendaji,
Uhai Tanzania, Dar es Salaam, Makao Makuu
0714418190;uhai1tz@yahoo.com ;

[Na 2B/2017DNMD]
Share on Google Plus

About UPStream Telecom

0 comments:

Post a Comment