Yaliyojiri katika mkutano wa bodi ya mikopo


TAARIFA YA YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO WA BODI YA MIKOPO

Kwa niaba ya wizara ya mikopo, Raisi wa serikali ya wanafunzi IFM-SO alifanikiwa kuhudhuria mkutano wa ufafanuzi wa mikopo ulioandaliwa na mkurugenzi wa BODI ya Mikopo tarehe 30 Oktoba 2016. BODI imesema kuwa mwaka huu inatarajia kutoa Mikopo kwa jumla ya wanafunzi  wapya  25,000 na mpaka Sasa imetoa kwa wanafunzi wapya 20,000 na kubakisha nafasi 5,000 kwa watu watakao kata rufaa na watu wenye mahitaji maalumu.

Raisi wa wanafunzi aliuliza yafutayo:
i)                 Swali: Kuna wanafunzi wanaoendelea 53 katika chuo cha usimamizi wa fedha ni yatima na wapo wenye maisha magumu na hawajapata mkopo Hali ya kuwa nao ni kipaumbele?
Jibu:
Wanafunzi hao wanatakiwa kukamilisha taarifa zao na kuziwasilisha kwa waziri husika wa mikopo wa serikali ya wanafunzi kwa kuwa hili ni suala la kiutawala watalishughulikia.

ii)     Swali: Je! BODI inataarifa juu ya suala la majina ya mwaka jana ya allocations yanayosambaa katika mitandao ya kijamii na kuhusishwa na zoezi la kujaza taarifa za kifedha kwenye akaunti za wanafunzi za BODI ya Mikopo?
Jibu:
Taarifa hizi ni za kizushi, BODI hawajatoa majina ya namna hiyo na majina yote  ya WANUFAIKA wapya wa Mikopo yapo katika tovuti ya BODI ya Mikopo wanafunzi watembelee kwenye tovuti.

iii)                Swali: Kwanini wanafunzi waliotokea diploma hawajapata mkopo?
Jibu:
Suala hili ni la kiutawala kwavile tumelifikisha BODI litashughulikiwa. (tumemuagiza waziri wa mikopo IFM kulifuatilia).

iv)           Swali: Kwanini wanafunzi wanaoendelea kufanyiwa uhakiki wa kifedha kupitia akaunti zao za BODI walizoombea na Kuna baadhi ya wanafunzi wanaweza kupoteza sifa za kupokea mikopo hiyo kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa na mkurugenzi wa BODI ya Mikopo, Je hawaoni kama wanawanyima haki ya kimsingi wanafunzi ambao tayari walikua wameingia mkataba Na Bodi ya mikopo?
Jibu: kila baada ya kipindi flani kupita serikali hufanya uhakiki wa wanufaika wa mikopo kwaajili ya kuboresha mifumo yao ya utoaji wa mikopo hiyo.

Raisi akaendelea kuhoji: kwanini mifumo hii isitumike kuanzia mwaka huu wa masomo na kuendelea maana vigezo vya mwaka Jana havifanani na mwaka huu. (mwaka Jana Kuna wanafunzi walipata mkopo kwa sababu ya ufaulu wao kuwa mzuri).
Maoni ya Raisi: Kwa upande wetu sisi bado tunaona BODI ya Mikopo Kuna haja ya kulifanyia tathmini upya suala hili ili lisiwaathiri wanafunzi wengi kisaikologia na kujiingiza kwenye vitendo viovu, tunaisihi sana BODI ya Mikopo kuliangalia upya suala hili ni mategemeo yetu kuwa litafanyiwa kazi.

v)       Swali: Kwanini Kuna poromoko la WANUFAIKA wapya wa mikop mwaka huu kulinganisha na mwaka Jana ambapo tulikua na WANUFAIKA zaidi ya 40,000 Lakin saivi ni WANUFAIKA 25,000 tu?
Jibu:
Sio walioomba wote mwaka huu wanasifa za kupewa Mikopo, waliopewa mikopo ndio wanasifa za kupokea mikopo hiyo.

vi)              Swali: Katika kujaza taarifa za kifedha kwenye akaunti za wanafunzi walizoombea mkopo wapo waliosahau neno la siri (Password), wanasaidiwaje?
Jibu:
BODI watatoa utaratibu kuanzia Jumatatu juu ya namna gani hao wanafunzi wafanye ili waweze kuingia kwenye akaunti zao.

RAI YA RAISI WA IFM-SO KWA WANAFUNZI WA IFM
Raisi anaomba wale wenye mahiitaji maalum hususan mayatima wafikishe taarifa zao kwa wizara ya mikopo kuanzia kesho (31/10/2016) ili tuwasihi BODI wawatambue wanafunzi hao wenye hali ngumu ya kimaisha lakini kwa wanaondelea wote wawe na mshikamano na kutusikiliza viongozi wenu tutaendelea kusimamia haki zenu kwa nguvu zetu zote.

Pia tunataraji kupokea vitabu vya WANUFAIKA wa Mikopo wanaoendelea hivi karibuni  ili watu wasaini meals and accommodation. 
Share on Google Plus

About UPStream Telecom

1 comments:

  1. Je! Unahitaji mkopo wa haraka ili uondole deni lako au unahitaji mkopo wa usawa ili kuboresha biashara yako? Umekataliwa na mabenki na mashirika mengine ya kifedha? Je! Unahitaji uimarishaji wa mkopo au mikopo? Utafute tena kama tuko hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani.

    Hii ni kampuni rahisi ya mkopo. Tunatoa mikopo kwa wale wanaopenda kiwango cha riba cha 2%. Mipangilio mbalimbali kutoka $ 5,000.00 hadi dola za dola 100,000,000.00.

    Mikopo yetu ni bima nzuri kama usalama wa juu ni kipaumbele chetu.

    Wasiliana nasi kwa barua pepe: oceanfmortgages@gmail.com


    Uzidi
    Max Bent
    oceanfmortgages@gmail.com
     
    Mikopo ya 2% ya awali na dhamana
    oceanfmortgages@gmail.com

    ReplyDelete