Taarifa kuhusu Fedha za field na utaratibu kwa walioko mikoani

TAARIFA JUU YA FEDHA ZA MAFUNZO YA VITENDO
  • Msisitizo kwa wanufaika wa mikopo waliopo maeneo ya karib na chuo juu ya fedha za mafunzo ya vitendo kuwa mnahitajika kufika chuoni kwaajili ya kufanikisha zoezi la kusaini fedha hizo ili ziweze kuingizwa kwenye akaunti zenu. Zoezi hili ni endelevu.
Malipo yatafanyika kama ifuatavyo: kila baada ya siku mbili wanafunzi watakao kuwa wamesaini, kundi hilo litachukuliwa na kuingiziwa hela zao (mfano: jumatatu na jumanne) baada ya hapo litafuata kundi lingine, vivo hivo baada ya siku mbili na kuendelea.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                         
Utaratibu kwa watu wa mikoani: 
  • Kwa walioko mikoani watasaidiwa kwa kutumia orodha ya watu wanaofanya field na project kwa kutumia orodha aliyonayo “field cordinator”, hili linafanikishwa kwa mujibu wa taarifa za mwanafunzi zilizojazwa kwenye akaunti yake ya kuwasilisha taarifa za field/ project kwenye mtandao.
  • Ili kupunguza hatari ya watu kutosaini, chuo kimeona ni busara kutumia matokeo ya wanafunzi ili kubaini walioshindwa kuendelea na masomo(walio discontinue) na kutowaekea fedha hizo.
  • Udanganyofu wa aina yoyote utabainika na mwanafunzi husika atachukuliwa hatua za kinidhamu.

  WIZARA YA MIKOPO
  IFM-SO 2016/17

Share on Google Plus

About UPStream Telecom

0 comments:

Post a Comment