Ratiba ya mazishi ya baba wa Katibu wa bunge la wanafunzi IFM


RATIBA YA MAZISHI YA BABA WA KATIBU WA BUNGE LA WANAFUNZI

26/08/2016 mnamo mida ya saa 2 usiku, serikali ya wanafunzi ikiongozwa na Ofisi ya raisi, ofisi ya waziri mkuu na Ofisi ya bunge kwa pamoja iliwasili nyumbani kwa mh. Allan (Mfiwa) na kutoa pole kwa wafiwa ikiwemo katibu wa bunge, mama yake mzazi pamoja na wadogo zake. Na kushirikiana na wafiwa katika mambo mbali mbali ya kimsiba.
Serikali ya wanafunzi ilikesha msibani na kuendelea na taratibu za kuandaa mazishi. Tarehe 28/08/2016 (Leo) Ratiba ya mazishi ni kama ifuatavyo:

Saa 5 asubuhi
Kuaga mwili wa baba yetu Mr. Mushi
Saa 6 mchana
Ibada kanisani alipokuwa akiabudu Mr. Mushi enzi za uhai wake.
Baada ya hapo mwili utasafirishwa kuelekea Moshi Machame

Mahali:
Mwili utaagwa Buza, kituo cha "Njia panda ya kwa Mwinyi", usafiri wa pikipiki mwendo wa dakika 2 "Argentina Kanisani". 

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na:
Naibu spika wa bunge: 0652 760 320 

Share on Google Plus

About UPStream Telecom

0 comments:

Post a Comment